Maria akiwa kwenye cherehani yake inayotumia mikono, ambayo anaitumia kushona nguo za wateja wake nyumbani kwake Mbagala.
Maria Patrick, alivyokuwa akitambaa kabla ya kuandikiwa makala na kuchapwa kwenye gazeti la Tanzania Daima na kupata wasamaria wema waliompatia baiskeli. hapa yupo karibu na nyumbani kwake Mbagala
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Bi. Usu Mallya akimkabidhi Maria Patrick baiskeli ya kumsaidia kutembea iliyotolewa msaada na Mchungaji wa kanisa la Pentekoste Tanzania Mch. Masanja hayupo pichani. Kushoto kabisa ni Bi. Lilian Liundi Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano TGNP na kulia kabisa ni MC wa tukio hilo Bi. Marie Shaba.